Picha za slide

Sunday, September 23, 2012

SATELITTE KURUSHWA KUTOKEA HAPA-BUNGA SDA CENTRAL CHURCH


WAATHIRIKA WA MOTO IKIZU WAPEWA MSAADA

Wanafunzi 100 wa Ikizu High School walioathirika kwa kupoteza mali zao kwenye ajali ya moto uliochoma mabweni mawili wamepewa msaada na shirika la msaada la Kanisa la Wa-adventista Wasabato (ADRA). Msaada huo uliotoka makao makuu ya kanisa la Wa-Adventista Wasabato, Njiro, Arusha, na kukabidhiwa kwa mkuu wa wilaya ya Bunda ndugu Joshua Mirumbe na mwenyekiti wa Konferensi ya Mara Mch. Daudi Makoye.

Mch. Daudi Makoye na Ndugu Mirumbe Wakikabidhi Wanafunzi Msaada

Katika hafla hiyo fupi, Mchungaji Makoye aliwashukuru wanafunzi, waalimu na wafanyakazi wa jumuia ya Ikizu kwa kuonesha ukomavu mkubwa na kuwa watulivu na kue- ndelea na masomo wakati tatizo lililowapata likishughulikiwa.
Aidha mkuu wa wilaya ndugu Mirumbe alilishukuru kanisa la Wa- Adventista Wasabato kwa kuwa makini kuwasaidia wanafunzi waliopoteza mali zao ili wasipoteze muda wa masomo. Pia alilisifu shirika la msaada la ADRA kwamba wanafanya kazi nzuri Africa nzima. Mr. Mirumbe aliwadokezea jumuia ya Ikizu kuwa amefanya mikutano na wafanya biashara wa wilaya ya Bunda ili wachangie kusaidia wanafunzi  wapate vitanda, vitabu, madaftari, sare na hata kukarabati jengo liloungua ili shule ya Ikizu irudi katika hali ya kawaida. Vifaa vilivyokabidhiwa kwa wanafunzi ni T-Shirts 175, sweta 122, suruali 94, mashati 82, Jackets 42, mablanketi 83 na "mats," vigodoro vidogo vya dharura 94; vyote vikiwa na thamani ya Tsh. 3, 736, 000.
Wanafunafunzi walionyesha furaha na kushangilia. Viongozi mbali mbali wa serikali walioandamana na mkuu wa wilaya waliwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii ili wachukue nafasi za mbalimbali taifani. Kwani hata mkuu wa wilaya mwenyewe aliwatia moyo kwamba alisoma katika shule ya Ikizu. Alisema, shule ya Ikizu ni kongwe na imetoa viongozi wengi hata katika ngazi ya taifa.

Jumuia ya Ikizu wakishuhudia kukabidhiwa msaada

Mwalimu Masasi anayekaimu ukuu wa shule alishukuru sana kanisa na uongozi wa serikali kwa kuonyesha moyo wa kujali shule Ikizu na maswala ya jamii.

Friday, September 21, 2012


SATELLITE DATES CHANGES-Breaking News

I have been informed this morning by Pr. Steve Bina, who is the ECD Satellite Cordinator, that the Kampala Net Event (satellite evangelism) of 2012 will now be uplinkeon from 29.09.2012 to 15.10.2012 instead of the previous dates (22.09.2012 - 06.10.2012) due to unavoidable technical reasons. We apologize for any inconvenience caused.

We are making announcement over Morning Star Radio regarding these changes. However I appeal to all of us to cooperate in passing this message to our downlink sites as fast as possible.
...

Kind Regards,

Pr Musa Mika
TU - Satellite Coordinator

Wednesday, September 19, 2012

UFUNGUZI WA MKUTANO KANISA LA WASABATO USHINDI (WATERFRONT HALL)









WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) Stephen Wassira ndie aliyekua mgeni rasmi siku hiyo ya ufunguzi akiwa na mwenyeji wake Askofu wa kanisa wa Wasabato Tanzania Mchungaji Dk Godwin Lekundayo.
Mh Steven Wassira alikagua gwaride ambalo lilikua likiendeshwa na wanafunzi wa Herritage.
Mkutano huo bado unaendelea (Waterfront hall)

Wednesday, September 12, 2012

Team to probe Ikizu school fire

Authorities in Bunda district, Mara region have formed a team of seven people to investigate the cause of a fire that gutted down two dormitories at Ikizu secondary school.

Bunda District Commissioner, Joshua Mirumbe, said the probe team will work under the district security committee. He said there are rumors that the fire was an act of malice and not an electrical fault as reported earlier by the school administration.
“The fire incident is suspected to be an act of sabotage… I want the probe team to look into the matter thoroughly,” he said.
Mirumbe said the team working with officials from the fire brigade department, is expected to complete its task within five days. He said the team is led by District Criminal Investigation Officer who is the chairman while other members will come from the police force, intelligence unit, village leaders and the school owner.
Mirumbe said the terms of reference include identifying the cause of the fire and making recommendations on how to avoid such an occurrence in future.
The incident occurred at around 9pm over the weekend. It was preceded by a huge blast before the fire spread quickly and burning down two dormitories with all the students' belongings.
Earlier, the Ikizu Secondary School Headmaster Emmanuel Masasi said the fire was caused by an electrical fault. He said the dormitories which were burnt down were used by100 Form One, Two and Three students.
He said the fire started when students were attending a preparatory session in the classrooms.
“No one was injured or killed during the incident,” he said, adding that all students will remain at the school while the administration communicate with their parents.
He called on Good Samaritans to volunteer support to the students since they have lost all their personal belongings.
SOURCE: THE GUARDIAN

Tuesday, September 11, 2012

Wednesday, September 5, 2012

JK MGENI RASMI KONGAMANO LA WASABATO-TAR17 HADI 28 SEPT




Rais Jakaya Kikwete, anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kongamano la maisha bora, lililoandaliwa na Kanisa la Waadiventista Wasabato kwa ajili ya kuwawezesha Watanzania kukabiliana na changamoto za maisha.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Kanisa hilo, Mchungaji Musa Mika, alisema kanisa lake linatambua wajibu wake kwa jamii na Serikali katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi.

Alisema ili kukabiliana na changamoto hizo, kanisa limeandaa kongamano ambalo litachukua siku kumi kuanzia Septemba 17 hadi 28, mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Kanisa la Waadventista kama sehemu ya jamii, tunatambua changamoto zinazoikabili nchi yetu, ingawa jitihada kubwa zinafanywa na Serikali, mashirika ya dini pamoja na asasi mbalimbali. 
 “Leo kuna watoto wanaoitwa wa mtaani ama idadi ya wanaolelewa na mzazi mmoja inaongezeka kutokana na kuongezeka kwa talaka na ndoa zisizo na furaha na hali hii huathiri malezi ya watoto, elimu yao na maendeleo ya taifa kwa ujumla,” alisema Mika.

Alisema kongamano hilo la maisha bora limelenga katika kupanua uelewa ambapo mada mbalimbali zitajadiliwa, ikiwamo ukimwi, maadili kwa jamii, uhuru wa dini, ujasiriamali, mazingira, athari za imani za uchawi na namna ya kudumisha amani katika nchi yetu.

Saturday, September 1, 2012

MAKAMBI MTAA UBUNGO-2012

Kambi la mtaa wa Ubungo mwaka huu 2012 lilianza tarehe 18 mwezi wa 8 na kumalizika tarehe 25, likiendeshwa na Pr Orlando(Mjamaika) anayefanya kazi kama senior pastor huko nchini marekani. lilijumuisha makanisa ya Externa, Mabibo, Kibangu juu, Mpakani na wenyeji Ubungo hill. aliyenyosha kidole ndiye Pr Orlando na pembeni yake alikuwa mfasiri Pr Mbuti kusekwa.



juu ni watu waliojitoa siku yamakambi na chini ni watoto na wazazi wao walipokuja kuwekwa wakfu