Picha za slide

Sunday, September 23, 2012

WAATHIRIKA WA MOTO IKIZU WAPEWA MSAADA

Wanafunzi 100 wa Ikizu High School walioathirika kwa kupoteza mali zao kwenye ajali ya moto uliochoma mabweni mawili wamepewa msaada na shirika la msaada la Kanisa la Wa-adventista Wasabato (ADRA). Msaada huo uliotoka makao makuu ya kanisa la Wa-Adventista Wasabato, Njiro, Arusha, na kukabidhiwa kwa mkuu wa wilaya ya Bunda ndugu Joshua Mirumbe na mwenyekiti wa Konferensi ya Mara Mch. Daudi Makoye.

Mch. Daudi Makoye na Ndugu Mirumbe Wakikabidhi Wanafunzi Msaada

Katika hafla hiyo fupi, Mchungaji Makoye aliwashukuru wanafunzi, waalimu na wafanyakazi wa jumuia ya Ikizu kwa kuonesha ukomavu mkubwa na kuwa watulivu na kue- ndelea na masomo wakati tatizo lililowapata likishughulikiwa.
Aidha mkuu wa wilaya ndugu Mirumbe alilishukuru kanisa la Wa- Adventista Wasabato kwa kuwa makini kuwasaidia wanafunzi waliopoteza mali zao ili wasipoteze muda wa masomo. Pia alilisifu shirika la msaada la ADRA kwamba wanafanya kazi nzuri Africa nzima. Mr. Mirumbe aliwadokezea jumuia ya Ikizu kuwa amefanya mikutano na wafanya biashara wa wilaya ya Bunda ili wachangie kusaidia wanafunzi  wapate vitanda, vitabu, madaftari, sare na hata kukarabati jengo liloungua ili shule ya Ikizu irudi katika hali ya kawaida. Vifaa vilivyokabidhiwa kwa wanafunzi ni T-Shirts 175, sweta 122, suruali 94, mashati 82, Jackets 42, mablanketi 83 na "mats," vigodoro vidogo vya dharura 94; vyote vikiwa na thamani ya Tsh. 3, 736, 000.
Wanafunafunzi walionyesha furaha na kushangilia. Viongozi mbali mbali wa serikali walioandamana na mkuu wa wilaya waliwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii ili wachukue nafasi za mbalimbali taifani. Kwani hata mkuu wa wilaya mwenyewe aliwatia moyo kwamba alisoma katika shule ya Ikizu. Alisema, shule ya Ikizu ni kongwe na imetoa viongozi wengi hata katika ngazi ya taifa.

Jumuia ya Ikizu wakishuhudia kukabidhiwa msaada

Mwalimu Masasi anayekaimu ukuu wa shule alishukuru sana kanisa na uongozi wa serikali kwa kuonyesha moyo wa kujali shule Ikizu na maswala ya jamii.

No comments:

Post a Comment